JE WAJUA PATRICK MATASI NI KIPA WA KWANZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KUMSHIKIA PENALTI MSHAMBULIAJI MATATA WA SENEGAL NA MABIGWA WATETEZI WA KOMBE LA UEFA LIVERPOOL,SADIO MANE?

Hivi karibuni mchezo wa kandanda imejulikana kuwa mchezo ambayo historia mengi huandishwa pale kisa ambacho kimewavutia na kutega wafuasi wengi duniani.
Hapo awali tumekuwa tukiwaona wachezaji na vilabu tofouti duniani hasa katika nchi za ulaya wakiingia katika vitabu vya kumbukumbu na kufanya vilibu hizo na wachezaji hao kuheshimika zaidi.Badhi ya wachezaji waliofahimika kuwika katika enzi zao na kusalia kwa vinywa vya wengi hadi wa Leo ni Kama vile Diego maradona ambaye alisaidia taifa lake la Argentina kunyakua kombe la dunia mwaka wa 1986. Alifahamika sana kwa welendi wake na kuchenga kwingi. Pele ambaye ni raia was Brazil pia ni mchezaji mwingine ambaye anakumbukwa na wengi. Nyota huyo aling`aa sana katika dimba la kuwania kombe la dunia katika miaka ya 60 na 70. Ni mchezaji mdogo duniani kuwahi shiriki katika dimba la kuwania kombe la dunia akiwa umri wa miaka 16. Aliweza kuisadia taifa lake kunyakua taji hilo mara tatu mnamo mwaka wa 1958, 1962 na 1970.

Historia haukukomea hapo hadi ulimwengu wa sasa wachezaji wanaendelea kuandikisha historia tofouti katika mchezo huu kwa mfano mwaka elfu mbili na tisa mchezaji;Christiano Ronaldo alingia katika vitabu vya kumbukumbu kuwa mchezaji ghali zaidi duniani. Real Madrid walimtwaa nyota huyo kutoka Manchester United kwa pauni milioni 94. Badhii ya wachezaji ambao bei yao ya uhamimisho ilitetemesha dunia ni Kama vile zinedine zidane (milioni 73.5), Zlatan Ibrahimovic ( milioni 69.5) Kaka wa  Brazil (65 milioni).

Mwaka jana beki wa Manchester United aliadikisha historia katika ulimwengu wa soka kuwa beki ghali zaidi duniani. Klabu ya Manchester United walimtwaa mchezaji huyo kutoka Leicester City kwa pauni milioni 80 na pauni milioni tano ambazo ziliongezeka baadae.
Continenti la Afrika haukuwachwa nyuma wachezaji wengi wameweza kuwika na kuonyesha umahiri jambo ambalo limewafanya wachezaji wao kwenda kuchezea vilabu kubwa katika nchi za ulaya.Wachezaji hao ni pamoja na Dider Drogba,Samuel Etoo, Adebayor, Solomon kolou,Riyad Mahrez,Sadio mane, Victor wanyama,Mabwana samatta na wengine wengi.
Mnamo tarehe mosi Julai mwaka wa 2019,katika uwanja wa 30 June Air Defence, katika mchuano wa kuwania kombe la Afrika AFCON, kipa wa timu la taifa la kenya Harambee Stars alingia katik a vitabu vya kumbukumbu Afrika mashariki na kati baada ya kumnyima bao la penalti nyota wa Senegal na mshambuliaji maarufu wa mabigwa watetezi wa kombe la UEFA bara ulaya Liverpool, Sadio mane. Patrick Matasi wa umri 32 ambaye amewahi kuichezea klabu tatu katika ligi ya Kenya ikiwemo Afc leopards (2011) Posta rangers (2015) na Tusker (2018) alionyesha umahiri mkuu wake katika mechi hiyo kisa ambacho kiliwafanya wakenya kumiminia sifa sufufu na kumfananisha na kipa nambari ya kwanza wa Manchester United David Dea Gea

Kipa wa Harambee stars Patrick Matasi akipangua penalti ya  mshambuliaji wa Senegal Sadio Mane katika
mchuano wa  kuwania kombe la AFCON  nchini mnamo tarehe mosi Julai 2019 katika uwanja wa 30 June Air Force
picha/AFP

















Patrick Matasi alionyesha mchezo mzuri na ya kuvutia baada ya kupakua mabao mengi ya nyota wa Senegal :Deny niang,Ismaila sarr,Henri saviet na kalidou koulibaly pamoja na penalti ya Sadio Mane katika kipindi cha kwanza na kufanya mechi hiyo kipindi Cha kwanza kuishia sare ya bila.Kipa huyo aliweza kusimulia jinsi alivyoweza kuipangua penalti kuwa alimwona macho yake Mane na hivyo alijua mahali angepiga mpira huo na akaweza kuipangua penalti hiyo
Ingawa timu ya Harambee stars hawakufuzu katika kundi C ,Patrick Matasi aliandikisha historia kuwa kumlinda lango wa kwanza katika mashindano hayo tangu mwaka  wa 2015 kuipangua penalti katika michuano hayo. Mchezo wake mzuri uliwafanya vilabu vingi kummezea mate mchezaji huyo wa taifa Harambee stars na anayechezea klabu ya Saint George SC nchini hivi sasa

@langat nathan7

Comments

  1. Lisukume gurudumu la spotii๐Ÿ˜‰๐Ÿ˜‰

    ReplyDelete
  2. Matasi alituwakilisha vizuri sana, kazi nzuri kaka

    ReplyDelete
  3. Matasi all the waaaaaaaaaay, kazi safi

    ReplyDelete
  4. kazi nzuri kwake matasi,....pia na wewe bro kazi nzuri๐Ÿ™๐Ÿ™ peperusha spoti⚽⚽⚽

    ReplyDelete
  5. Aliandikisha historia Kali bruh ..keep them coming through

    ReplyDelete
  6. Nice Article bro...Keep going#Norman

    ReplyDelete
  7. Excellent analysis of best players, keep it up,,

    ReplyDelete
  8. Swafy kabisa ila wakati mwingine soma kazi yako vizuri kabla ya kuichapisha ili kuepuka makosa madogomadogo ya sarufi kuzuia kutomchosha msomaji

    ReplyDelete
  9. Cool Sana๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

    ReplyDelete
  10. Cool Sana๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

    ReplyDelete

Post a Comment